0


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kushoto) akizungumza na wananchi walio fika katika viwanja vya Mnazi Mmoja kupata vipimo na kupatiwa ushauri na Madaktari kutoka Hospitali Mbalimbali Jijini Dar es Salaam.

Wananchi wakiwa na watoto wao katika viwanja vya Mnazi Mmoja 

Wananchi wakiwa katika mistari ambao hawajapata namba 

Mkuu wa Idara ya magonjwa ya Dharura na Ajali Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Juma Mfinanga akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa zoezi la kupima vipimo kwa wananchi bure lililoratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kwa kushirikiana na madaktari kutoka hospitali mbalimbali za Dar es Salaam ikiwemo, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aga Khan Hospital, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ikiongonzwa na Rais wa Chama cha Madaktari Figo Tanzania na pia ni Daktari Bingwa wa Figo Dk. Onesmo Kisanga 

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace (kushoto) Magembe akiwaonyesha jambo wananchi waliojitokeza kupata huduma ya vipimo kutoka kwa madaktari wa hospitali mbalimbali ikiwemo Hospitali ya Taifa Muhimbili mkoa wa Dar es Salaam, zoezi lililoratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, lililofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini humo.

Kutokana na mwitikio wa wananchi, huenda siku zitaongezwa baada ya Mkuu huyo kujadiliana na madaktari hao.

Septemba 25 ilikuwa ndiyo siku ya kuhitimisha zoezi hilo.


Wafanyakazi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja 

Zuhura Shaba (54) akiwa amebebwa na baadhi ya Madaktari na wafanyakazi wa Afya baada ya kujikuta amepoteza fahamu mara baada ya kufika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam.

Baada ya muda na mpiga picha hizi alibahatika kuongea naye na kuanza kusema kwa utaratibu kinachomsumbua na kueleza mengi. Alisema yeye ni Mtoto wa 7 na baba yake enzi za uhai wake miaka ya nyuma alishika nyadhifa mbalimbali serikalini kama, Waziri wa Afya, Meneja Mkonge Tanga, Mbunge.

Alisema anamshukuru Mkuu wa Mkoa na "Mungu amuongoze kwa kila anachokifanya kwa Jamii ya Kitanzania," na kumshukuru Rais wa Tanzania, "kwa kumpa maono ya kumchagua kijana huyu, Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa," na kuishukuru timu nzima ya Madaktari kwa moyo wao kuona jamii ya Kitanzania bado ina hali duni na, "kushirikiana na Mkuu wa Mkoa kutuletea zoezi hili, nashukuru baada ya kujikuta napoteza fahamu nimejikuta nipo katika chumba huduma ya haraka na kupata huduma na sasa najiona ninanafuu."


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi Sophia Mjema (kushoto) akishiriki zoezi la kugawa namba kwa wananchi walioitikia wito wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam 

Baadhi ya wananchi wakiwa wamenyoosha mikono wakitarajia kupata namba kwa ajili ya kupatiwa huduma ya vipimo 


Askari Polisi akizungumza na baadhi ya Wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Mnazi Mmoja 




Joyce Mgeta akipatiwa vipimo na Dk. Daniel Chacha (kushoto) mara baada kujikuta anaishiwa nguvu ghafla akiwa katika foleni ya kusubiri kupata namba. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dk. Juma Mfinanga 


Picha zote na maelezo: UMBEA MFULULIZO.

Chapisha Maoni

 
Top