0
Karibu ndege 15 zinazosafirisha miraa huwasili mjini Mogadishu kila siku
Kenya inasema kuwa inafanya kila iwezalo kuishawishi serikali ya Somalia kubatilisha uamuzi wa kuzipiga marufuku ndege zinazosafirisha mirraa.
Marufuku hiyo ilitangazwa na Somalia wiki iliyopita na imeathiriwa biashara ya thamani ya karibu dola nusu milioni kwa siku.
Soko la miraa la Beerta lilikuwa bila shughuli wiki iliyopita kufuatia marufuku hiyo
Msemaji wa serikali ya Kenya amesema kuwa marufuku hiyo haikutokana na ziara ya hivi majuzi ya afisa wa cheo cha juu wa kenya, katika eneo lililojitenga nchini Somalia la Somaliland kutafuta soko kwa miraa.
Amesema kuwa Rais Uhuru Kenyatta sasa anaingilia kati suala hilo.

Chapisha Maoni

 
Top