Baadhi ya wabunge wameibua hoja tofauti kwenye mitandao ya kijamii baada
ya Rais John Magufuli kupokea ripoti ya mchanga wa madini Ikulu, leo.
Katika akaunti yake ya Twitter, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu
ameandika, “pongezi kwa kazi nzuri iliyofanywa na tume.”
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe katika ukurasa wake wa Twitter
ameandika, “utafiti unapingwa kwa utafiti. Kwa sasa Kamati ya Mruma Ndio
rejea sahihi kwenye suala la mchanga na hivyo nakubali mapendekezo
yaliyomo.”
Naye, Naibu Waziri Afya, Hamis Kigwangalla katika akaunti yake yaTwitter
ameandika, “sishangai kumsikia Rais wetu akisema 'wasomi' tumeiangusha
nchi. Kwa kila namna tunapaswa kujitazama sana.”
Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ameandika, “nimemsikiliza
mheshimiwa Rais na kuendelea kuielewa nia yake njema ya kuisaidia nchi
yake. Tuko pamoja na ninakuunga mkono.”
Chapisha Maoni